Proverbs 1:24-27


24 aLakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita
na hakuna yeyote aliyekubali
niliponyoosha mkono wangu,

25 bkwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote
na hamkukubali karipio langu,

26 cmimi nami nitawacheka katika maafa yenu,
nitawadhihaki wakati janga litawapata:

27 dwakati janga litawapata kama tufani,
wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli,
wakati dhiki na taabu zitawalemea.

Copyright information for SwhKC